Tuesday, May 8, 2012

TANGAZO KUHUSU PRE- ENTRY PROGRAM SAUT

                                                   TANGAZO
 Chuo cha Mtakatifu Agustino Tanzania kinawatangazia nafasi za kujiunga na Remedial Programme kwa mwaka wa masomo 2012/2013.Kozi hii ni kwa ajili ya wale wote ambao alama zao hazifiki kiwango cha 4.5 katika kidato cha sita, ili kuwawezesha kupata elimu ya ili iwasaidie kuendana na wanafunzi wenzao waliopata alama zaidi ya 4.5 katika kidato cha sita. Sifa za Muombaji: 1. Awe amemaliza kidato cha sita. 2. Awe na Principal Passes 2 (mfano: EE, DE, CE, DD, EEE na masomo mengine kuwa na S) ambazo zinafikia 2.5 hadi 4 kwenye masomo mawili ya kidato cha sita 3. Gharama ni Tshs. 390,000/= (Tuition Fee) kwa miezi 3, malazi (accommodation) ni Tshs. 70,000/=, chakula ni kujitegemea. 4. Wale wote wenye sifa hizo watakaochaguliwa na TCU kuja SAUT watatakiwa kufika chuoni miezi mitatu kabla ya tarehe ya kujiunga chuoni kwa ajili ya kuanza masomo ya remedial. 5. Kozi hii itaanza tarehe 2/7/2012. Fomu zinapatikana ofisi ya Admissions office na kwenye tovuti (www.saut.ac.tz). Baada ya kumaliza kujaza fomu zirudishwe ofisi ya Admissions-SAUT. Wahitimu wataruhusiwa kujiunga na vyuo vyote vilivyo chini ya SAUT ambavyo vinatoa programmes husika. NB: WAOMBAJI PIA WANAPASWA KUOMBA KUPITIA TCU Wote mnakaribishwa. Admissions Officer

No comments:

Post a Comment